Tanzania
This article was added by the user . TheWorldNews is not responsible for the content of the platform.

Bajeti Ya Serikali Ya Marekani Chupuchupu Kukwama – Yapata Idhini Ya Matumizi Ya Wiki Sita Tu

Spika wa Bunge la Republican Kevin McCarthy.

Baraza la wawakilishi la Marekani Septemba 30, 2023 limepitisha mswaada wa sheria wa kuifadhili serikali kuu kwa siku 45 na hivvo kuepusha kufungwa kwa shughuli za serikali. Mswaada huo ulipitishwa kwa theluthi mbili ya Wabunge wote.

Mswaada huo ulipitishwa kwa kura 335 dhidi ya 91.

Muda wa matumizi ya fedha za serikali ulitarajiwa kumalizika leo Jumamosi Septemba 30 kabla ya usiku wa manane. Awali wabunge wa mrengo mkali wa kulia katika chama cha Republican walitishia kutoidhinisha mswaada wa kuifadhili serikali ikiwa serikali ya Rais Joe Biden haitapunguza kwa kiasi kikubwa matumizi yake hasa kwenye miradi ya lishe kwa watoto wa shule na familia zenye kipato cha chini, pia kusitisha mswaada wa dola bilioni 6 kwa Ukraine.

Mswaada huo unatakiwa kupitishwa na Baraza la Seneti na kusainiwa na Rais Joe Biden kuwa sheria.

Mamilioni ya wafanyakazi wa serikali kuu wakiwemo wanajeshi walikuwa katika hatari ya kutolipwa mishahara yao, maelfu ya wengine wangelazimika kufanya kazi bila malipo endapo shughuli za serikali zingefungwa.

spoti pesa below post

Global Publishers and General Enterprises Limited is a registered private company dealing in publishing of weekly Swahili newspapers in Tanzania, namely; Uwazi, Ijumaa, Championi, Amani, Risasi & Ijumaa Wikienda.