Tanzania
This article was added by the user . TheWorldNews is not responsible for the content of the platform.

Mchungaji Mwakipesile Ahukumiwa Kifungo Cha Miaka Mitatu Jela

Mbarikiwa Mwakipesile

Mchungaji Mbarikiwa Mwakipesile (39), baba mzazi wa Sifa Bujune, Muimbaji wa Injili anayetuhumiwa kusambaza uongo kutokana na Wimbo wake wa “Mnatuona Nyani Tu”, amehukumiwa kifungo hicho na Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya kwa kosa la kuendesha Huduma ya Kiroho bila kibali

Akizungumza na JamiForums, Wakili Boniphace Mwabukusi amesema “Kweli amehukumiwa lakini Mchungaji alifuata machakato wa kuomba vibali japo Serikali ndio ilikuwa ikichelewesha. Pia, Sheria inasema mtu ambaye yupo katika mchakato wa maombi hawezi kushtakiwa.”
Ameongeza “Adhabu aliyofungwa nayo ina faini na kifungo, Hakimu ametoa adhabu ya kifungo bila faini. Tunatarajia kukata rufaa Jumatatu (Oktoba 2, 2023).”

spoti pesa below post

Global Publishers and General Enterprises Limited is a registered private company dealing in publishing of weekly Swahili newspapers in Tanzania, namely; Uwazi, Ijumaa, Championi, Amani, Risasi & Ijumaa Wikienda.