Tanzania
This article was added by the user . TheWorldNews is not responsible for the content of the platform.

Rais Samia: Tuna ‘Crisis’ Ya Umeme, Tunafanya Ukarabati Wa Mashine – Video

Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza mara baada ya kuwaapisha Viongozi mbalimbali Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Septemba, 2023.

Rais Samia Suluhu Hassan amempa miezi sita Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO ), Gissima Nyamo-Hanga kushughulikia tatizo la kukatika kwa umeme ili kuondoa kadhia hiyo kwa wananchi.

Nyamo-Hanga ameteuliwa kuchukua nafasi ya Maharage Chande ambaye ameteuliwa kuwa Postamasta Mkuu, Shirika la Posta Tanzania.

Akizungumza kuhusu changamoto ya kukatika kwa Umeme katika Mikoa mbalimbali Nchini, Rais Samia Suluhu Hassan amesema mitambo haikufanyiwa maboresho kwa muda mrefu, hivyo maboresho yanapofanyika baadhi huzimwa ambapo husababisha upungufu wa umeme.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Bw. Gerson Partinus Msigwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Septemba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Bi. Bahati Ibrahim Geuzye kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Septemba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Bw. Mohamed Jumanne Gombati kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Septemba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Said Othman Yakubu kuwa Balozi kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Septemba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Bw. John Ulanga kuwa Balozi kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Septemba, 2023.
Viongozi mbalimbali wakila Kiapo cha Maadili ya Utumishi wa Umma Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Septemba, 2023.


spoti pesa below post

Global Publishers and General Enterprises Limited is a registered private company dealing in publishing of weekly Swahili newspapers in Tanzania, namely; Uwazi, Ijumaa, Championi, Amani, Risasi & Ijumaa Wikienda.