Tanzania
This article was added by the user . TheWorldNews is not responsible for the content of the platform.

Harmonize amedhulumu haki za Ibraah kwa kutomlipa ndani ya miezi 6 akisema alikuwa anampima??

Kupitia kwenye kipindi cha RECAP & MANDO @el_mando_tz ameizugumzia kauli ya Harmonize akilinnganisha na mahojiano aliyoyafanya Ibraah na SNS kuhusu kutokulipwa ndani ya miezi 6 ambapo ilipelekea kukaa kimya kimuziki.

Kauli ya Harmonize anasema kuwa alikuwa anampima Ibraah kuhusu ukomavu kwenye muziki lakini majibu ya Ibraah anasema ametoa ngoma ya HAPA ili kulinda kipaji chake kisife.

Ikumbukwe kuwa Ibraah baada ya kuachia ngoma ya HAPA aliweka wazi kuwa kwa sasa anapitia wakati mgumu sana kwenye muziki wake na baada ya kuulizwa alijibu hakulipwa malipo ya kazi zake ndani ya miezi 6.

Kauli hiyo imewashtua wengi kwani waliamini kuwa kutokulipwa kwa Ibraah ni kwa sababu Harmonize alisema kuwa anawadai Ziiki lakini kauli ya Harmonize ndio ikawaacha wengi midomo wazi baada ya kusema kuwa Ibraah hakulipwa kwa sababu yeye alikuwa anampima.

@el_mando_tz anasema kauli ya Harmonize ni mbaya sana hasa kwenye kuathiri kipaji cha msannii wako ukidai ulikuwa unampima kama amekomaa kwenye muziki.

Ibraah ni mfanyakazi wa konde Gang maana na mkataba, je Harmonize baada ya kumaliza kumpima Ibraah atamlipa stahiki zake za miezi 6?? na Je kuathiri kipaji cha Ibraah kwa madai ya kumpima malipo yake ni yapi??

Dondosha comment yake hapa chini, unahisi Harmonize alikuwa sasa kwa kauli ile??