Tanzania
This article was added by the user . TheWorldNews is not responsible for the content of the platform.

Muigizaji na Muongozaji wa Filamu G Marimuthu Afariki

Tasnia ya Filamu nchini India inaomboleza kifo cha Muigizaji na Muongozaji maarufu wa Filamu G Marimuthu, aliyefariki dunia Septemba 8, 2023 kwa mshtuko wa moyo.

Marimuthu aliyekuwa akifanya kazi na tasnia hiyo kwa upande wa lugha ya Tamil, alianguka akiwa katika studio ya televisheni huko Chennai na alitangazwa kuwa amefariki baada tu ya kufikishwa hospitali.

Muigizaji huyo mkongwe ameigiza zaidi ya filamu 50 na hadi mauti yanamkuta alikuwa akirekodi kazi ya tamthilia ya Ethirneechal (Swimming Against The Tide)ambamo alikuwa mmoja wa waigizaji wakuu.

Moja ya Filamu zake za mwisho kuigiza ni “Jailer” ambayo ni ya tatu kwa mafanikio katika Filamu za India kwa mwaka huu.

spoti pesa below post

Global Publishers and General Enterprises Limited is a registered private company dealing in publishing of weekly Swahili newspapers in Tanzania, namely; Uwazi, Ijumaa, Championi, Amani, Risasi & Ijumaa Wikienda.